Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Maswi (kulia) akipokea baadhi ya vifaa vya TEHAMA kutoka kwa Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe. Angela Kairuki, hafla ya makabidhiano ya vifaa hivyo imefanyika leo 15 Disemba, 2025 Mtumba jijini Dodoma.
Picha ya pamoja ya ujumbe wa Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari ukiongozwa na Waziri Mhe. Angela Kairuki (katikati) pamoja na ujumbe wa Wizara ya Katiba na Sheria ukiongozwa na Katibu Mkuu, Ndg. Eliakim Maswi (wa pili kulia) baada ya kupokea vifaa vya TEHAMA vilivyotolewa na Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari kwa lengo la kuimarisha mfumo wa upatikanaji haki nchini.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Homera (Kulia) akikabidhi cheti cha kuzaliwa kwa Bi. Fatuma Madiga baada ya Uzinduzi wa mpango wa kutoa vyeti vya kuzaliwa ndani ya saa 48 ambapo cheti hicho pia kimepatikana ndani ya muda huo.
Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Dkt. Juma Homera (Wa pili Kulia) akizindua mpango wa kutoa vyeti vya kuzaliwa ndani ya saa 48, wengine ni Naibu Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Zainab Katimba (Wa Kwanza kulia), Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA Frank Kanyusi na Naibu Kabidhi Wasii Mkuu Bi. Irene Lesulie (Wa kwanza kushoto) katika hafla iliyofanyika Desemba 12, 2025 Jijini Dar Es Salaam
Heri ya Maadhimisho ya miaka 64 ya Uhuru wa Tanzania Bara
Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe. Dkt. Juma Zuberi Homera, akizungumza na wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara, Menejimenti na baadhi ya watumishi wa Wizara ya Katiba na Sheria, mara baada ya kupokelewa na kukabidhiwa ofisi rasmi, Mtumba jijini Dodoma, 18 Novemba 2025.
Katibu Mkuu Wizara ya Katiba na Sheria, Ndg. Eliakim Chacha Maswi, akitoa neno la ukaribisho kwa Waziri na Naibu Waziri wa Katiba na Sheria (hawapo pichani) mara baada ya viongozi hao kuwasili na kupokelewa katika ofisi za Wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma, 18 Novemba, 2025
Picha ya pamoja, Viongozi wa juu wa Wizara ya Katiba na Sheria, Waziri Dkt. Juma Zuberi Homera (wa pili kulia) Naibu Waziri, Mhe. Zainab Athuman Katimba (wa tatu kulia), Katibu Mkuu, Ndg. Eliakim Chacha Maswi (wa kwanza kulia) na Naibu Katibu Mkuu, Dkt. Franklin Jasson Rwezimula (wa kwanza kushoto) mara baada ya Waziri na Naibu Waziri kuwasili rasmi katika ofisi za Wizara, Mtumba, 18 Novemba, 2025.
Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Juma Zuberi Homera (katikati) na Naibu Waziri Mhe. Zainab Athuman Katimba wakiwa katika picha ya pamoja na Wakuu wa Taasisi zilizo chini ya Wizara na Menejimenti ya Wizara ya Katiba na Sheria mara baada ya kupokelewa rasmi katika ofisi za wizara zilizopo Mtumba jijini Dodoma, 18 Novemba, 2025
Nukuu za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Novemba 14, 2025 Dodoma.